HABARI

 

Friday, March 8, 2013

UCHAGUZI WA KENYA: DONDOO ZA YANAYOJIRI

0 Comments

Shughuli ya kuhesabu kura za urais katika uchaguzi wa Kenya, inajikokota , huku ikizua hali ya taharuki katika nchi ambayo ingali na makovu ya ghasia za baada ya uchaguzi wake wa mwaka 2007.
Wagombea wakuu wa urais katika uchaguzi huo, Raila Odinga na Uhuru Kenyatta anayesubiri kesi yake katika mahakama ya kimataifa ya ICC, kufuatia tuhuma za kuhusika na ghasia za mwaka 2007.
Bwana Kenyatta yuko mbele kwa hesabu ya kura za urais dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga.
Upande wa Odinga unasema kwa hujuma imefanywa katika shughuli ya kuhesabu kura hizo katika ukumbi wa Bomas, viungani mwa Nairobi.
Uchaguzi ulifanywa chini ya katiba mpya iliyoundwa ili kuzuia kutokea tena kwa ghasia zizoshuhudiwa mwaka 2007, kufuatia uchaguzi uliokumbwa na utata...Hii imesemekana kuwa sababu moja ya wapiga kura kuchanganyikiwa

Kwa nini tume kachelewa kutangza matokeo?

Mfumo wa Elektroniki- uliotumiwa kwa mara ya kwanza katika uchaguzi wa Kenya. Mfumo huo uligoma siku ya Jumanne.
Hii haikumshangaza mwangalizi mkuu wa kikosi cha Jumuiya ya madola, Festus Mogae, rais wa zamani wa Botswana alisema kuwa, "bado hatujafikia kiwango cha nchi za Magharibi. ''

Shunguli ya kuhesabu kura ilikumbwa na changamoto kubwa kwani mitambo ya Tume ya uchaguzi iligoma
Hatujui kilichosababisha mitambo kugoma, lakini naibu mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, Lilian Mahirie alisema kuwa huenda mtambo ulivamiwa.
Na kwa sababu ya hilo, kura sasa zinahesabiwa kwa mikono moja baada ya nyingine.
Tume ya uchaguzi inatumai kuweza kumaliza shughuli hiyo na kutangaza matokeo rasmi Ijumaa, lakini kulingana na sheria ina hadi tarehe 11 kutangaza matokeo hayo.
Haya yote yanajiri wakati Kenya ikiwa inatumia mfumo mpya wa kuhesabu kura wa elektroniki ambao uligoma katika vituo vingi vya kupigia kura, na sasa wamelazimika kutumia sajili za wapiga kura.

Mzozo unatokana na nini?

Unatokana na kura ambazo zinasemekana kuharibika na hivyo haziwezi kuhesabiwa kama kura sahihi na ikiwa zinaweza kuhesabiwa sawa na kura zingine zisizo na makosa yoyote.
Muungano wa Bwana Odinga CORD unataka kura hizo kuhesabiwa lakini muungano wa Kenyatta JUBILEE umepinga hatua kama hiyo.
Mgombea mwenza wa Kenyatta, William Ruto ameteta akisema kuwa kupiga kura sahihi kunamaanisha kuweka kwenye kijisanduku kinachostahili, wakati, afisaa mkuu katika muungano wa Raila, Franklin Bett, amesema kuwa kura yoyote iliyowekwa katika sanduku la kura lazima iwe sehemu ya kura zote zilizopigwa.
Baadhi ya wagombea tayari wamejulishwa matokeo yao, hawa wakiwa magavana, maseneta na waakilishi wa wanawake
Wadadisi wanasema kuwa chini ya katiba mpya, kura sio lazima ziwe sahihi bora tu zimepigwa na kuingizwa ndani ya sanduku ya kura.
Wadadisi wanasema kuwa chini ya katiba mpya, kura sio lazima iwe sahihi ndio zihesabiwe, kura yoyote inaweza kuhesabiwa kinyume na mambo yalivyokuwa hapo nyuma.
Ikiwa pande hizo mbili zitakosa kusuluhisha mzozo huu basi huenda mmoja akalazimika kwenda katika mahakama kuu.
Swala hili ni muhimu kwa sababu katiba inasema kuwa ili kuzuia duru ya pili, mgombea lazima ashinde zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa katika duru ya kwanza na takriban asilimia 25 ya kura katika nusu ya kaunti zote.

Ni kura ngapi zilizoharibika zinazozozaniwa?

Hadi Jumanne , matokeo ya mwanzo yalionyesha kuwa idadi ya kura zilizoharibika ilikuwa asilimia sita, idadi ambayo ilikuwa nyingi kuliko kura alizopigiwa mgombea anayeshikilia nafasi ya tatu, Musailia Mudavadi.
Wadadisi wanasema kuwa kulikua na kura nyingi sana zilizoharibika kwa sababu wakenya walikuwa na mfumo mpya wa kupiga kura wakiwapigia kura wagombea sita na ndio maana wakachanganyikiwa sana.
Wapiga kura walimchagua rais, mbunge, mwakilishi wa wanawake, magavana, maseneta na mwakilishi wa kaunti
Ilipofika Alhamisi idadi ya kura zilizoharibika ilikuwa imeshuka pakubwa.

Mamilioni ya wakenya walijitokeza asubuhi na mapema kupiga kura
Haijulikani ni kwa nini.
Maafisa wa uchaguzi, sasa wanasema kuwa wamelegeza msimako kuhusu kura zilizoharibika, na sasa wanazijumlisha na kura sahihi hasa ikiwa iliwekwa kwenye sanduku isiyostahili mfano kura ya Gavana kuwekwa katika sanduku ya kura za rais.
Baadhi ya kura pia zilikataliwa kwa sababu alama aliyoweka mpiga kura kutoka nje kidogo ya boxi. Baadhi wanasema ikiwa nia ya mpiga kura inaweza kujulikana basi, kura hiyo inaweza kuhesabiwa.
Pia kumekuwa na mtafaruk kuhusu tofauti kati ya kura iliyokataliwa na kura sahihi.
Kulingana na sheria, kura inakataliwa ikiwa pamoja na mengine haina alama ya kuithibitisha kuwa kura sahihi.
Lakini kura iliyoharibika ni ile ambayo mpiga kura aliweka alama ambayo haistahili karibu na mgombea aliyetaka kumpigia kura. Kwa hili mpiga kura anaweza kuomba kura nyingine wakati ile ya kwanza aliyoiharibu ina kuwa kura inayokataliwa.

Je wakenya wamechukulia vipi kucheleweshwa kwa matokeo?

Wakati shughuli hii ikiendelea kucheleweshwa, ndio wakenya nao wanazidi kuwa na wasiwasi mkubwa, sababu ambayo inaweza kusababisha mgogoro mkubwa.
Siku ya Alhamisi mgombea mwenza wa Odinga, Kalonzo Musyoka, alisema kuwa kumetokea hujuma dhidi ya matokeo yao.
Milolongo mirefu ilishuhudiwa katika vituo vya kupigia kura
Awali,muungano wa Jubilee, ulituhumu Uingereza kwa kuingilia uchaguzi huo ili kumnyima ushindi, madai ambayo nchi hiyo imekanusha.
Kenyatta anakabiliwa na kesi ya uhalifu wa kivita katika mahakama ya kimatifa ya uhalifu wa kivita, akihusishwa na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2007 ambapo takriban watu zaidi ya 1,000 waliuawa na wengine laki sita kuachwa bila makao.
Kabla ya uchaguzi Muungano wa Ulaya ulisema utapunguza uhusiano na Kenya ikiwa itamchagua rais anayehusishwa na ICC, wakati naibu katibu wa Marekani kuhusu maswala ya Afrika, Johnnie Carson, alionya kuwa wakenya wajiandae kwa athari za kumchagua mtu fulani.

Nini umhumi wa Kenya Kimataifa?

Ina uchumi mkubwa wa Afrika Mashariki na hupokea msaada mkubwa kutoka nchi za Magharibi.
Shughuli ya kukusanya matokeo kura za urais imeanza upya zaidi ya masaa arobaini na nane baada ya wakenya kupiga kura
Pia ina jeshi lenye nguvu zaidi katika ukanda huo pamoja na kutuma maelfu ya wanajeshi nchini Somalia kupambana dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu.
Kwa hivyo, Ulaya na Marekani zinajipata katika hali ngumu kisiasa ikiwa Kenyatta anayekabiliwa na kesi ICC atachaguliwa kama rais mpya wa nchi.
Barani Afrika huenda kuchaguliwa kwake kusizue mtafaruku kwani muungano wa Afrika unaopinga mahakama ya ICC unamuunga mkono Rais Bashir wa Sudan ambaye anasakwa na mahakama hiyo.
Viongozi wa Afrika wameituhumu mahakama ya ICC, kwa kuwa na mapendeleo dhidi ya bara la Afrika na kupuuza makosa ya jinai yanayofanywa na viongozi wengine wa dunia.

0 Comments:

Post a Comment