- Tangazo la NSSF
- Mgari wa Obama
- Ulinzi mkali wakati wa ujio wa Obama
- Dege la Obama
- Rais Kikwete na Obama katika Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam
Tangazo la NSSFMore
Gari lililombeba Barack Omaba alipokuja TanzaniaMore
Ulinzi mkali Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam, alipokuja ObamaMore
Dege alilotua nalo Obama TanzaniaMore
Obama akiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Kikwete baada ya kutua TanzaniaMore
TangazoMore
Saturday, October 12, 2013
Thursday, October 10, 2013
ZIARA YA ZITTO KABWE KANDA YA MAGHARIBI, JIMBO LA IGALULA
Siku
ya 5 ya ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi imetufikisha Jimbo la
Igalula, wilaya ya Uyui. Tumekutana na wananchi katika vijiji vya
Goweko, Loya, Miswaki, Miyenze na Kigwa.
Tumezungumza kuhusu
changamoto ya usafiri wa Reli, wafugaji kunyanyaswa na watendaji wa kata
na askari kwa kunyanganywa mifugo, zao la Tumbaku, maji safi na salama
na suala la jumla la Katiba na mchakato wa kuandika katiba.
Kimsingi shughuli za kiuchumi za wananchi ni kubwa na hasa Kilimo na
mifugo. Hata hivyo ukosefu wa miundombinu unafanya wananchi wasipate
thamani ya mazao yao na jasho la kazi zao.
Nilipofika Kijiji cha Loya nimeona eneo kubwa lina miti ya mihama.
Wananchi wanatumia tu mihama wakati wa njaa na mara nyingi matunda haya
yanaharibika tu. Lazima matunda haya yana matumizi yake ya kiviwanda
maana ‘kernel’ yake ina mafuta. Na hili ni swali aliloacha Mh Zitto Kabwe Nani anajua matumizi ya Mihama?
IMETAYARISHWA NA DJ SEK BLOG P.O.BOX Dar es salaam IT DEPARTMENT
Wednesday, October 9, 2013
ZANU-PF: WAAFRIKA VIPUUZENI VYAMA VYA UPINZANI
*Chadai ni mawakala wa Nchi za Magharibi
*Chahoji, kama Mugabe ni Mzee sana, mbona Malikia Elizabeth ni mzee zaidi ya Zimbabwe?
BASHIR NKOROMO, DSM
WATANZANIA na Waafrika kwa jumla wametakiwa kutovitilia maanani vyama vya upinzani kwa madai kuwa ni vya kibinafsi na havina mwelekeo wa kuwasaidia wananchi.
Wametakiwa kuendelea kukiamini na kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi (CCM), ili kiendelee kuongoza Tanzania kwa kuwa ndicho chama chenye sera na mtazamo wa uhakika wa maendeleo.
Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Chama tawala cha Zambia, ZANU-PF, Didymus Mutasa, katika mkutano wa sita wa Makatibu Wakuu wa Vyama vilivyokuwa vya ukjombozi kusini mwa Afrika,
uliofanyika leo, katika hoteli ya Kunduchi Beach, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Mutasa alisema vyama vya upinzani havina hadhi ya kuaminika sana kwa wananchi kwa sababu si vyama makinikutokana na uanzishwaji wake kuwa ni wa ubabaishaji jambo ambalo linavikosesha misingi ya kuweza kuleta maendeleo.
“Afrika hakuna vyama vya upinzani, Watanzania wasikubali kabisa, kwa kuwa vyama hivyo havina mwelekeo hasa kutokana na kutokuwa na mizizi katika uanzishwaji wake tofauti na vyama utawala ambavyo pamoja na kuanzishwa kwa lengo la kuzikomboa nchi zao lakini pia viliweka misingi ya kuinua uchumi,’’alisema.
Alizilaum nchi za Magharibi, akisema ndizo zimeleta utitiri wa vyama vya upinzani kwa lengo la kutafuta mianya ya kuja kunyonya na kupora rasilimali zilizo ndani ya Afrika, na kusisitiza kuwa waafrika wasikubali kuvipa nafasi.
Kuhusu chama chake cha ZANU-PF kuendelea kutwaa madaraka ya uongozi nchini Zimbabwe kupitia chaguzi mbalimbali, ukiwemo ulimalizika hivi karibuni na Rais Robert Mugabe kushinda Katibu Mkuu huyo alisema, umetokana na Wazimbabwe kutokubali kuwapa wapinzani nchi na pia ZANU-PF kusimamia vizuri sera ya uwekezaji.
“Tuna hakika tunapendwa na wazanzibabwe, hasa kutokana na serikali kuwa wa wazi na kuhakikisha inasimamia rasilimali za nchi na hata kusikiliza vilio vyao. Hivyo, ushindi wetu ni sauti ya Wazimbabwe,’’ alisema.
"Hata kelele zao hasa za kuhoji kuwa Rais Mugabe ni mzee mwenye umri mkubwa, mbona wao wanasahau kuwa Malkia Elizabeth ni mzee kuliko hata nchi yenyewe ya Zimbabwe achilia mbali Rais Mugabe?, alisema na kuongeza;
“Malkia ni Mzee kuliko Zimbabwe yenyewe na bado ni malkia wa Uingereza. Hivyo Mugabe ni Rais wetu na bado wazimbabwe wanampenda".
Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti na mwenyekiti wa Mkutano huo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdurahman Kinana alisema miongoni mwa mambo ambayo Makatibu wakuu watajadili kwa kina ni namna ya kuwatafutia fursa vijana, ili waweze kushiriki katika masuala mbalimbali ya nchi zao ikiwemo kushika nafasi za uongozi.
Vyama vilivyoshiriki Mkutano huo, ni CCM (Tanzania), SWAPO cha Namibia, ZANU-PF cha Zimbabwe, MPLA cha Angola, FRELIMO cha Msumbiji na ANC cha Afrika Kusini.
Read more...
*Chahoji, kama Mugabe ni Mzee sana, mbona Malikia Elizabeth ni mzee zaidi ya Zimbabwe?
Katibu Mkuu, ZANU-PF,Mutasa, akizungumza leo |
WATANZANIA na Waafrika kwa jumla wametakiwa kutovitilia maanani vyama vya upinzani kwa madai kuwa ni vya kibinafsi na havina mwelekeo wa kuwasaidia wananchi.
Wametakiwa kuendelea kukiamini na kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi (CCM), ili kiendelee kuongoza Tanzania kwa kuwa ndicho chama chenye sera na mtazamo wa uhakika wa maendeleo.
Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Chama tawala cha Zambia, ZANU-PF, Didymus Mutasa, katika mkutano wa sita wa Makatibu Wakuu wa Vyama vilivyokuwa vya ukjombozi kusini mwa Afrika,
uliofanyika leo, katika hoteli ya Kunduchi Beach, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Mutasa alisema vyama vya upinzani havina hadhi ya kuaminika sana kwa wananchi kwa sababu si vyama makinikutokana na uanzishwaji wake kuwa ni wa ubabaishaji jambo ambalo linavikosesha misingi ya kuweza kuleta maendeleo.
“Afrika hakuna vyama vya upinzani, Watanzania wasikubali kabisa, kwa kuwa vyama hivyo havina mwelekeo hasa kutokana na kutokuwa na mizizi katika uanzishwaji wake tofauti na vyama utawala ambavyo pamoja na kuanzishwa kwa lengo la kuzikomboa nchi zao lakini pia viliweka misingi ya kuinua uchumi,’’alisema.
Alizilaum nchi za Magharibi, akisema ndizo zimeleta utitiri wa vyama vya upinzani kwa lengo la kutafuta mianya ya kuja kunyonya na kupora rasilimali zilizo ndani ya Afrika, na kusisitiza kuwa waafrika wasikubali kuvipa nafasi.
Kuhusu chama chake cha ZANU-PF kuendelea kutwaa madaraka ya uongozi nchini Zimbabwe kupitia chaguzi mbalimbali, ukiwemo ulimalizika hivi karibuni na Rais Robert Mugabe kushinda Katibu Mkuu huyo alisema, umetokana na Wazimbabwe kutokubali kuwapa wapinzani nchi na pia ZANU-PF kusimamia vizuri sera ya uwekezaji.
“Tuna hakika tunapendwa na wazanzibabwe, hasa kutokana na serikali kuwa wa wazi na kuhakikisha inasimamia rasilimali za nchi na hata kusikiliza vilio vyao. Hivyo, ushindi wetu ni sauti ya Wazimbabwe,’’ alisema.
"Hata kelele zao hasa za kuhoji kuwa Rais Mugabe ni mzee mwenye umri mkubwa, mbona wao wanasahau kuwa Malkia Elizabeth ni mzee kuliko hata nchi yenyewe ya Zimbabwe achilia mbali Rais Mugabe?, alisema na kuongeza;
“Malkia ni Mzee kuliko Zimbabwe yenyewe na bado ni malkia wa Uingereza. Hivyo Mugabe ni Rais wetu na bado wazimbabwe wanampenda".
Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti na mwenyekiti wa Mkutano huo, Katibu Mkuu wa CCM, Abdurahman Kinana alisema miongoni mwa mambo ambayo Makatibu wakuu watajadili kwa kina ni namna ya kuwatafutia fursa vijana, ili waweze kushiriki katika masuala mbalimbali ya nchi zao ikiwemo kushika nafasi za uongozi.
Vyama vilivyoshiriki Mkutano huo, ni CCM (Tanzania), SWAPO cha Namibia, ZANU-PF cha Zimbabwe, MPLA cha Angola, FRELIMO cha Msumbiji na ANC cha Afrika Kusini.
Tuesday, October 8, 2013
NAIBU KATIBU MKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI MH. MWIGULU NCHEMBA (MB) AUNGURUMA NCHINI UINGEREZA NA KUONYESHA UKOMAVU WAKE KIFIKRA.
· “Mabadiliko hayatakuja kwa kubadilisha vyama bali ni nia zenu {Mindset) zikifanywa kuwa mpya na mapenzi ya nchi
yenu.”
Naibu Katibu
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa na Mbunge wa Iramba Magharibi Mh. Mwigulu
Lameck Nchemba akisisitiza Jambo katika hotuba yake aliyoitoa hapa nchini
Uingereza iliyojaa mapenzi na Tanzania
zaidi ya Itikadi na kupokelewa vyema na watanzania wengi hapa UK .
SOMA HABARI KAMILI
Katika hali
iliyotajwa kuwa ni ya furaha, kutokana
na changamoto zilizokuwepo siku ya jumamosi jijini Leicester Uingereza, kijana
shupavu na “JEMBE” la kujivunia katika Taifa la Tanzania Naibu Katibu Mkuu wa
CCM Taifa, na Mbunge wa Ilamba Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Lameck Nchemba
akiambatana na mshauri wa Rais mheshimiwa Rajabu Luhwavi, kwa pamoja waliweza
kutoa majibu ya changamoto nyingi zinazolikabili Taifa kwa watanzania wengi
waliojitokeza katika mkutano mkubwa uliohudhuriwa na watanzania wengi kutoka
maeneo mbali mbali ya Uingereza.
Ujasiri,
uwazi na ukweli wa mambo ya kiutendaji katika taifa letu ndio hasa imekuwa ni
chachu na kivutio kikubwa kwa watanzania wengi waliohudhuria mkutano huo mkubwa
jiji Leicester ambapo Mh. Mwigulu Nchemba aliweza kuweka wazi mengi ambayo
serikali imeweza kuyafanya katika upande wa Elimu, Miundo mbinu na huduma za afya kwa watanzania pia kutoa
kasoro katika maeneo yanayokuwa vikwazo katika kutoa huduma bora.
“Nchi yetu
ipo katika mchakato wa kupata katiba mpya, mojawapo ya mambo ambayo tunayafanyia
kazi ni suala la uraia pacha. Ni pendekezo lililowakirishwa na Chama Cha
Mapinduzi katika baraza zake za uchangiaji maoni ya Katiba mpya. CCM inawajali
watanzania wote hivyo ikaona ni vyema na nyinyi mlioko ughaibuni kupata fursa
sawa za kimaendeleo katika nchi yenu” alisema Mhe. Mwigulu Nchemba.
Mheshimiwa
Nchemba aliendelea na kusema kwamba nchi yetu inapita katika kipindi cha
mabadiliko. Idadi ya watanzania imeongezeka kwa kiasi kikubwa na wengi wa
ongezeko hili ni vijana ambao ni watafutaji na wajasiliamali wengi. Kuna haja
kubwa kama chama kubuni taratibu nzuri za
kimaendeleo ili kuendana na wimbi hili la ongezeko la watu.
Mheshimiwa Nchemba
kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi aliwasihi watanzania waishio Uingereza kutumia
upeo (Exposure) waliyonayo katika kulisaidia taifa kupiga hatua zaidi za
kimaendeleo kuliko kuwa na ushabiki wa siasa kama ilivyo kwa baadhi ya
wanasiasa nyumbani na badala yake wawe chemichemi ya mawazo ya kimaendeleo
katika nchi yao .
Watanzania
mlioko nje mna nafasi kubwa ya kuchangia mawazo ya kujenga taifa lenu la
Tanzania, nitawakilisha hoja yenu ya kupatiwa njia ya kuwakilisha mawazo yenu
ama jambo lolote lenye busara na utendaji wa mabadiliko katika nchi yetu ya Tanzania
ili pia mpate fursa ya kuwakilisha maoni na hoja za haja za kuleta mabadiliko. Kutokuwa
na jukwaa lenu la kuwakilisha hoja zenu za kamandeleo ni kosa. Wazo lolote la
kujenga lazima liwakirishwe katika vikao
rasmi kama mchango wa CCM diaspora, liongeza Mheshimiwa Nchemba.
Tengenezeni
ajenda kulingana na ukomavu na upana wenu wa kimawazo ambao mnaupata katika
nchi hizi za Magharibi ambazo zimepiga hatua kubwa za kimaendeleo kutokana na
desturi zao za kuthamini, kujituma na
kutenda kazi zao kwa uadilifu mkubwa kwa mapenzi na nchi zao ili kuchangia utekelezaji wa sera ya chama
katika nchi yetu kwenye sekta mbalimbali za afya, elimu, miundombinu , sheria
n.k. na mimi naahidi tutatengeneza na kuboresha uwanja mzuri wa mawasiliano
kati yetu aliongeza Mheshimiwa Mwigulu Nchemba.
Mheshimiwa
Nchemba pia alisisitiza upendo na umoja baina ya watanzania na kuwaomba wawe
kitu kimoja na akawataka wana CCM Uingereza kuwa chachu ya kuwaunganisha
watanzania wote bila kujali itikadi za kisiasa na vyama vyao. Mheshimiwa
Nchemba pia amekuwa akikonga nyoyo za watanzania wengi kulingana na utashi na ufahamu
wa kujibu maswali kiufasaha, wazi na kwa uhakika pale alipoulizwa katika mikutano yake
iliyofanyika katika majiji ya Leicester, Northampton
na London
nchini Uingereza.
Katika
mkutano uliofanyika jijini Leicester watanzania wengi waliuliza maswali
yanayohusu Katiba , Utawala wa Sheria wenye haki sawa kwa wote kama ilivyo
katika nchi za kimagharibi, Uraia pacha, Kurugenzi inayoshughulikia masuala ya
Diasprora ambayo badala ya kuwa kiunganishi imekuwa ni kikwazo kikubwa kwa
wanadiaspora kutokana huduma mbovu zenye kutokujali na majivuno kutoka kwa
watendaji wake wakuu, Tunashauri watendaji katika kitengo hiki watokane na
wanadiaspora wenyewe kwani upeo (exposure) wao kiutendaji utaleta ufanisi
kuliko ilivyo sasa hivyo kuleta mchango wao kwa maendeleo ya Taifa. Pia Watanzania
hao na wana CCM wameishauri serikali kubadirisha taratibu zake za kiajira katika
Balozi zetu za nje kwa kuwatumia watanzani wenyeji wa maeneo hayo ili kupunguza
mzigo wa gharama serikali, kuongeza ufanisi kwani uelewa wa kufanya kazi katika
mazingira wanayoishi wanaufahamu vyema zaidi kuliko kuleta watendaji wote
katika Balozi zetu kutoka nyumbani.
Vilevile
katika mkutano uliofanyika jijini Northampton siku ya Jumapili, mengi ya maswali
yaliyoulizwa na watanzania waishio katika jiji hilo ni kama katika masuala ya usalama wa nchi na raia
wake dhidi ya matukio ya tindikali na majanga ya mabomu kule Arusha, tukio la
kigaidi hivi karibuni nchini Kenya na utayari wa nchi yetu katika kukabiliana
na wimbi kama hilo endapo litatokea nchini kwetu, mikakati ya kupambana na
madawa ya kulevya pamoja na lile gonjwa sugu la rushwa.
Akijibu kwa
ufasaha maswali hayo Mheshimiwa Rajab Luhwavi ambaye anaambatana na Naibu
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Mheshimiwa Mwigulu Nchemba, katika ziara hii, alianza
kwa kuwahakikishia usalama wa taifa Watanzania waliofika katika mkutano huo na
kuwaondoa hofu hiyo. Na kuwajulisha kwamba serikali imeweka mikakati madhubuti
ya kupambana na uhalifu wa aina hiyo na kwamba taratibu za lazima zinafanyika
na hali ni shwari.
Imetumwa kwetu na: Abraham Sangiwa –
Deputy Secretary Ideology and Publicity
Chama Cha
Mapinduzi Uingereza (CCM UNITED
KINGDOM )
Tarehe 08.10.2013.
Subscribe to:
Posts (Atom)