HABARI

 

Tuesday, January 1, 2013

MGEJA: MBOWE AMEVUNJA DEMOKRASIA

0 Comments

SHINYANGA, Tanzania 
   KAULI iliyotolewa hivi karibuni na mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe  kwamba Dkt. Wilbroad Slaa ndiye atakayekuwa mgombea urais mwaka 2015 imetafsriwa kuwa ni uvunjaji wa demokrasia ndani ya chama hicho .

  Kauli hiyo imeelezwa kuwa inapingana na dhana nzima ya demokrasia nchini na kwamba Mbowe ameonesha wazi kwamba CHADEMA si chama cha kidemokrasia kama kinavyojieleza na kujinadi kila siku mbele ya watanzania na badala yake kinaendeshwa kifamilia.

  Akizungumza na viongozi mbalimbali wa madhehebu ya dini na wazee wa mjini Kahama juzi katika hafla fupi ya kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013 katika ukumbi wa Kahama Hotel mjini hapa,. mwenyekiti wa Taasisi ya Tanzania Mzalendo Foundation, Khamis Mgeja alisema taasisi yake imeshitushwa na kauli hiyo.

 Mgeja alisema haamini kwamba chama ambacho kinachohimiza kila siku suala la demokrasia nchini, mwenyekiti wake asimame hadharani na kumtangaza mwanachama fulani kwamba ndiye atakayekuwa mgombea wa nafasi ya urais badala ya maamuzi hayo kufanywa na vikao halali vya kikatiba. 

 Alisema Taasisi yake ambayo moja ya shughuli zake ni kuimarisha suala la demokrasia nchini na utawala bora imesikitishwa na kauli ya Mbowe na kwamba ameonesha jinsi gani chama chake kinavyokandamiza demokrasia ndani ya chama ambapo ameifafananisha kauli hiyo na kauli zinazotolewa na madikteta duniani.

  “Hii kauli ni katika jitihada za Mbowe kuikandamiza demokrasia ndani ya chama, ni wazi sasa CHADEMA kimepoteza mwelekeo, si muda muda mrefu kitasambaratika,”  

“Hizi ni njama za wazi za kutowapa nafasi wanachama wengine wasiweze kujitokeza kuomba na kugombea nafasi hiyo kupitia CHADEMA, sisi hatuamini kwamba Dkt. Slaa ndiye anayefaa peke yake, maana chama hicho kina watu wengi wanaoweza kujipima kuwania nafasi hiyo kama vile Zitto (Kabwe) na Shibuda (John),” alisema Mgeja.  

Mgeja ambaye pia  ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) na mwenyekiti wa CCM mkoani Shinyanga alisema baada ya kauli hiyo sasa haitokuwa rahisi kwa wana CHADEMA wengine kama vile Zitto na Shibuda kuweza kuwania nafasi hiyo ambao tangu awali walitangaza nia ya kugombea. 

 “Kauli ya Mbowe sisi Tanzania Mzalendo Foundation tunaiita kuwa ni kauli ya kibabe na kidikteta na ambayo moja kwa moja inawapokonya haki yao ya kikatiba Zitto na Shibuda, hawatoweza tena kuitumia, maana tayari mwenyekiti wao Taifa ameishatoa msimamo wa chama,”

 “Nafikiri ni katika mbinu za kuwawekea vizingiti mapema, maana hata muasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei amesikika akiunga mkono kauli ya Mbowe ambaye tunafahamu wazi kuwa huyo ni baba mkwe wake, na ni wazi kuwa msingi wa kauli hiyo ni kuwadhibiti Shibuda anayetokea kanda ya ziwa na Zitto anayetokea Kigoma,” alieleza Mgeja. 

 Hata hivyo Mgeja alimtaka Mbowe aelewe kuwa kauli yake hiyo mbali ya kuvunjavunja mfumo wa demokrasia nchini lakini pia inawanyima wanachama wengine wa CHADEMA haki yao ya kikatiba na kwamba kwa kufanya hivyo ameichezea katiba ya chama chake.

  Akizungumzia hali ya amani na utulivu uliopo hivi sasa nchini, Mgeja alisema ipo hatari ya hali hiyo kutoweka iwapo serikali haitochukua mapema hatua za kuwakemea wale wote ambao wameanza kueneza maneno ya uchochezi ambayo yanaweza kusababisha kutokea kuvunjika kwa utulivu uliopo.

  Alisema moja ya watu wanaoeneza maneno ya uchochezi ni viongozi wa CHADEMA ambao mara kwa mara katika mikutano yao wamekuwa wakitishia kuingia msituni pale watakapobaini matakwa yao yameshindwa na hawakuungwa mkono na watanzania. 

 Mgeja alisema kauli ya hivi karibuni ya viongozi wa CHADEMA kwamba mwaka 2013 Tanzania haitotawalika ni kauli hatarishi kwa amani na utulivu uliopo hapa nchini hivi sasa na kwamba inapaswa kukemewa vikali na kila mpenda amani. 

“Hizi kauli kwa kweli ni kauli hatari sana kwa mstakabali wa nchi yetu, haziendani na utamaduni wa watanzania, nchi yetu imezoea amani na utulivu na imekuwa na umoja wa kitaifa daima, na ni mfano wa kuigwa na mataifa mengine duniani,”

  “Ni vizuri zikakemewa na kila mtanzania, lakini hawa wenzetu pia wamekuwa na tabia ya kutoa kauli za zinazomdhihaki  Rais wa nchi aliyeko madarakani, ambaye alikula kiapo halali cha kuwatumikia watanzania wote bila ya ubaguzi wowote, huu ni utovu wa nidhamu, ni vizuri wakakemewa mapema,” alisema Mgeja. 

 Alisema inavyoelekea hivi sasa CHADEMA kimeanza kupoteza mwelekeo kiliokuwa nao na kinaelekea kuporomoka mporomoko mkubwa, na kwamba kinapoamua kuachana na demokrasia ndani ya chama kama lilivyo jina lake ni wazi wanachama watasambaratika haraka.  

“Ni wakati muafaka hivi sasa kwa watanzania kuchukua tahadhari kubwa na viongozi hawa wa CHADEMA, waache ile tabia ya kuwaunga mkono na kuingia mabarabarani kupinga mambo bila ya wao wenyewe (wananchi) kuchunguza sababu ya wao kuandamana, watajikuta  wakiwahangaikia watu wachache kwa maslahi yao binafsi,” alisema.

   Akizungumza katika hafla hiyo, Al Haji Alley Juma kwa niaba ya wazee wa mji wa Kahama alisema ni vizuri sasa Msajili wa vyama vya siasa nchini, John Tendwa awe macho na kufuatilia kwa karibu kauli mbalimbali zinazotolewa na viongozi wa vyama vya siasa ambazo zinaweza kuchangia kuvunjika kwa haliya amani na utulivu.   uchochezi huku wakitoa maneno ya kumdhalilisha Rais, hawa wasiruhusiwe kuichezea amani tuliyonayo, wadhibitiwe mapema na ikibidi watajwe hadharani,” alisema mchungaji Mlekwa. 
Read more...